Timu za Manchester zatamba England
26 Februari 2018Mshambuliaji wa United Romelu Lukaku aliwanyamazisha wale waliokuwa wanazungumzia uwezo wake wa kukucheza vyema dhidi ya timu mahiri kwa kuwa alifunga goli la kwanza la Manchester United na kuunda la pili lililotiwa kimiani na Jesse Lingard.
Chelsea walikuwa kifua mbele katika mechi hiyo kupitia Willian ila United walijizoazoa na kuebuka na ushindi mbele ya mashabiki wao na sasa wanaishikilia nafasi ya pili nyuma ya Manchester City katika jedwali la ligi ya nchini England huku Chelsea wakiwa wanaendelea kuyadidimiza matumaini yao ya kumaliza miongoni mwa timu nne bora.
Manchester City wao walikuwa wanacheza fainali ya taji la Carabao uwanjani Wembley dhidi ya Arsenal na walikuwa na kazi rahisi walipowapepeta tatu mtungi hao the gunners Sergio Aguero, nahodha Vincent Kompany na David Silva wakiwafungia City mabao yao na kumpa Pep Guardiola kikombe chake cha kwanza tangu kuchukua uongozi wa klabu hiyo.
Mwandishi: Jacob Safari/DPAE/Reuters
Mhariri: Josephat Charo