1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Syria: Mbinyo wazidi kwa Urusi na China

6 Juni 2012

Urusi imesema kuwa rais Bashar al-Assad anaweza kuondoka madarakani kama sehemu ya suluhisho la kumaliza umwagakaji damu uanaoendelea nchini Syria ,nayo Saudi Arabia imeitaka Urusi kutounga mkono utawala huo ►

https://p.dw.com/p/158jc
Anti-government protesters raise their arms as part of a funeral procession for Yaser Raqieh, whom protesters say was killed by forces loyal to Syria's President Bashar al-Assad, near Hama June 5, 2012. REUTER/Handout (SYRIA - Tags: CIVIL UNREST POLITICS) FOR EDITORIAL USE ONLY. NOT FOR SALE FOR MARKETING OR ADVERTISING CAMPAIGNS. THIS IMAGE HAS BEEN SUPPLIED BY A THIRD PARTY. IT IS DISTRIBUTED, EXACTLY AS RECEIVED BY REUTERS, AS A SERVICE TO CLIENTS
Mapambano yanaendelea nchini SyriaPicha: Reuters

Urusi imo katika mbinyo unaoongezeka ili kuunga mkono kuondoka kwa Bashar al-Assad madarakani kama hatua ya mwanzo katika makubaliano ya amani ambayo yatasabasha watu wa karibu na Assad kuchukua madaraka ya mpito, chini ya makubaliano kama yaliyopatikana nchini Yemen na kuungwa mkono na umoja wa mataifa ya serikali ya mpito nchini Yemen mwaka huu.

Naibu waziri wa mambo ya kigeni wa Urusi Gennady Gatilov amesema , " Hatujawahi kusema ama kusisitiza kuwa ni lazima Assad abaki madarakani ifikapo mwishoni mwa utaratibu wa kisiasa",

Suala hili ni lazima lisuluhishwe na Wasyria wenyewe, ameongeza naibu waziri huyo akinukuliwa na shirika la habari la Urusi ITAR-TASS.

Taarifa hiyo ni moja kati ya taarifa za wazi kabisa za Urusi juu ya nafasi ya Assad tangu waziri wa mambo ya kigeni wa nchi hiyo Sergei Lavrov kukataa wazi kuunga mkono utawala wa Assad wakati alipofanya ziara nchini Syria Februari mwaka huu.

Urusi yakata mkutano wa kimataifa

Wakati huo huo waziri wa mambo ya kigeni wa Urusi Sergei Lavrov ametoa wito leo wa kuitishwa mkutano wa kimataifa kuhusu mzozo wa Syria utakaojumuisha mataifa ya Iran na Uturuki kwa lengo la kuunga mkono mpango unalega lega wa amani uliofikiwa kwa upatanishi wa mjumbe wa kimataifa Kofi Annan.

Taarifa hiyo imekuja wakati Urusi na China , ambazo zimezuwia hatua zinazoongozwa na mataifa ya magharibi dhidi ya Syria, kuanza mazungumzo yanayohusu kufikisha mwisho karibu miezi 15 ya ghasia ambazo zimesababisha watu zaidi ya 13,500 nchini Syria kuuwawa na karibu watu wengine 47 wamepoteza maisha jana Jumanne.

epa03249669 Chinese President Hu Jintao (R) and Russian President Vladimir Putin (C) walk together after they reviewed an honor guard during a welcoming ceremony for the Shanghai Cooperation Organization (SCO) summit at the Great Hall of the People in Beijing, China, 05 June 2012. Russian President Vladimir Putin arrived in Beijing for talks that were expected to focus on Syria, bilateral energy cooperation, and other international issues. EPA/MARK RALSTON / POOL +++(c) dpa - Bildfunk+++
Rais wa China Hu Jintao na Wladimir Putin wa UrusiPicha: picture-alliance/dpa

Marekani yataka ushirikiano zaidi

Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Hillary Clinton amezitaka China na Urusi kuwa sehemu ya suluhisho la mzozo wa Syria baada ya kukubaliana kufanyakazi kwa karibu zaidi katika umoja wa mataifa.

Balozi wa China katika umoja wa mataifa Li Baodong amesema kuwa juhudi za kumaliza mauaji zimeingia utata na kwamba majeshi ya serikali na waasi ni lazima yasitishe mapigano. Msemaji wa wizara ya mambo ya kigeni ya China Liu Weimin amesema.

"China na Urusi sinapinga vikali mataifa ya kigeni kuingilia kati nchini Syria na zinapinga mabadiliko ya utawala kwa kutumia nguvu".

Kuongezeka kwa matumizi ya nguvu na ghasia nchini Syria kumesababisha mataifa ya Kiarabu kuelezea wasi wasi wao juu ya uwezekano wa mpango wa amani wa umoja wa mataifa , ambao umefikiwa kwa upatanishi wa mjumbe wa kimataifa Kofi Annan.

Waziri mkuu mpya Syria

epa03251027 An undated handout photo made available by Syria's Arab News Agency SANA on 06 June 2012 shows former Syrian agriculture minister Riyad Farid Hijab, who was entitled to form the new government by Syrian President Bashar al-Assad on 06 June 2012. Hijab, 46, holds a doctorate in agricultural engineering and is a member of the Baath Party. He served as the secretary general of the Arab Baath Party branch at Deir Ezzour. He was the governor of Latakia before being nominated as an agriculture minister, reported state news agency SANA. EPA/SANA HANDOUT HANDOUT EDITORIAL USE ONLY/NO SALES
Waziri mkuu mpya wa Syria Riyad Farid HijabPicha: picture-alliance/dpa

Wakati huo huo rais Bashar al-Assad amemteua waziri wa zamani wa kilimo nchini humo na ambaye ni mshirika wake wa karibu Riyad Hijab kuwa waziri mkuu mpya. Anachukua nafasi inayoachwa wazi na Adel Safar ambaye aliteuliwa kushika wadhifa huo Aprili mwaka jana.

Mwandishi : Sekione Kitojo /dpae / ape/ afpe

Mhariri: Moahammed Abdul-Rahman