SPIN BOLDAK: Mshambuliaji ajiripua miongoni mwa polisi
6 Julai 2007Matangazo
Si chini ya askaripolisi 10 wa Afghanistan wameuawa na wengine 11 wamejeruhiwa katika shambulio la kujitolewa muhanga.Shambulio hilo limetokea kwenye kituo cha ukaguzi kusini-mashariki ya Afghanistan.Mshambulizi huyo alijiripua alipokuwa amekaa pamoja na polisi mjini Spin Boldak karibu na mpaka wa Pakistan. Msemaji wa Taliban amedai kuwa wamehusika na shambulizi hilo.