1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Rwanda yaadhimisha miaka 50 ya uhuru ''shingo upande''

2 Julai 2012

Rwanda imeadhimisha miaka 50 tangu ilipopata uhuru na maadhimisho hayo ambayo hayakuwa na shamra shamra kubwa yalifanywa sambamba na mengine ya miaka 18 tangu kusimamishwa kwa mauaji ya kimbari.

https://p.dw.com/p/15Pys
Rais Paul Kagame wa Rwanda
Rais Paul Kagame wa RwandaPicha: picture-alliance/dpa

Uhuru wa Rwanda ulipatikana tarehe 1 Julai mwaka 1962, kutoka kwa wakoloni wa kibelgiji. Hata hivyo, kwa miaka mingi siku hiyo huadhimishwa shingo upande, kwani viongozi wa serikali na baadhi ya raia huamini kuwa uhuru huo hauna maana, kwani ulipatikana wakati wa mgawanyiko mkubwa ambao ulipelekea kwenye mauaji ya kimbari ya mwaka 1994. Mnamo miaka ya hivi karibuni, siku hiyo imekuwa ikijumuishwa na sherehe za siku ya ukombozi, tarehe 4 Julai, ambayo mauaji ya kimbari ya mwaka 1994 yalisimamishwa, na chama tawala kwa sasa, RPF, kuchukua hatamu za uongozi.

Siku kuu ya ukombozi hupewa umuhimu zaidi

A Rwandan worker arranges human bones and skulls in Kigali, Rwanda, Thursday, April 6, 2000. Across this Central African nation, survivors of the 1994 genocide are excavating pits, yards and septic tanks, retrieving corpses of some of the more than half-million victims for a dignified reburial. (AP Photo/Sayyid Azim)
Ruanda VölkermordPicha: AP

Hii ndo siku inayozungumzwa na serikali ya hapa bila chembe yoyote ya manung'uniko na hivyo inapewa umuhimu mkubwa.Sheikh Abdulkarim Harerimana ni mwanasiasa mkongwe nchini Rwanda anasema kuadhimisha siku ya ukombozi kuliko ile ya uhuru ni suala lililoanza hata abla ya serikali hii kuingia madarakani.

''Tangu mapinduzi ya kijeshi ya mwaka 1973 yaliyofanywa na aliyekuwa rais wa Rwanda Habyarimana Juvenal, siku kuu ya uhuru iliambatanishwa na siku kuu ya mapinduzi hayo, ambayo ilifanyika tareke 5 Julai. Kwa hiyo siku ya mapinduzi hayo ilipewa uzito kuliko siku kuu ya uhuru kwa sababu Habyarimana alidai aliikomboa nchi kutokana na matatizo makubwa ya kisiasa''. Alisema Sheikh Harerimana.

Maadhimisho bila shamra shamra

Bildergalerie Ruanda Versöhnung Bild 2 Ehrung für Ruandas Helden Jedes Jahr am 1. Februar gedenken die Ruander ihrer Helden. Im Amahoro Stadion in Kigali findet ein riesiges Spektakel mit Tanz, Musik und Reden statt. Zu den Helden zählt auch eine Gruppe von Schülern. Die Inyange Secondary School wurde während des Genozids von den Interahamwe überfallen und die Schüler sollten sagen, ob sie Hutu oder Tutsi sind. Als sie sich weigerten, wurden viele von ihnen umgebracht. *** Bilder von James Nzibavuga, Mai 2009
Flash-Galerie Ruanda Versöhnung Bild 2Picha: James Nzibavuga

Ingawa kila mwaka siku ya uhuru haipewi uzito mkubwa kama ile ya ukombozi. Mwaka huu hali ni tofauti kidogo angalau yanaonekana maandalizi ya hapa na pale, pengine kwa sababu sababu sasa maadhimisho ni ya nusu karne. Alipoulizwa iwapo Rwanda itasherehekea miaka huo tangu kuondoka kwa wakoloni, rais wa Rwanda Paul Kagame alisema itaadhimishwa ''kwa namna fulani'', pengine ili kutoa nafasi ya kuutafakari uhuru huo.

Ijapokuwa wengi hawapendi kutoa maoni yao waziwazi lakini wanapendekeza kwamba siku ya uhuru iwe inapewa umuhimu mkubwa kwa kuwa inasalia kuwa na hadhi yake kama siku ya uhuru wa taifa.

Mwandishi: Sylvanus Karemera/Dw-Radio-Kigali

Mhariri: Daniel Gakuba