RIYADH: Waumini waliokwenda kuhiji wamefariki katika ajali ya basi
9 Desemba 2006Matangazo
Waingereza 2 wamefariki na wengine 25 wamepelekwa hospitali wakiwa na majeraha,kufuatia ajali ya basi lililokuwa likisafirisha watu waliokwenda kuhiji nchini Saudi Arabia.Basi hilo lilipata ajali kama kilomita 90 kaskazini ya mji wa Jeddah lilipokuwa likisafiri kati ya miji takatifu ya Medina na Mekka.Kila mwaka kiasi ya Waingereza 25,000 huenda kuhiji Mekka.