1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Riadh. Pelosi analiza ziara yake ya mashariki ya kati.

5 Aprili 2007
https://p.dw.com/p/CCCJ

Spika wa baraza la wawakilishi nchini Marekani , Nancy Pelosi kutoka chama cha Democratic , amekutana na baraza la kisiasa la ushauri nchini Saudi Arabia wakati wa ziara yake ya mashariki ya kati.

Pelosi alitembelea baraza hilo la ushauri wa kisiasa ambalo huteuliwa na mfalme Abdullah wa Saudi Arabia .

Pelosi amewasili nchini humo akitokea Syria, ambako amekaidi sera za Ikulu ya Marekani kuelekea mashariki ya kati kwa kukutana na rais wa Syria Bashar al-Assad.

Pelosi amesema Assad amemwambia kuwa Syria iko tayari kuanza tena majadiliano ya amani na Israel. Serikali ya rais wa Marekani imemshutumu Pelosi kwa kufifisha juhudi za kuutenga utawala wa rais Assad kwa madai ya kuunga mkono ugaidi pamoja na kile kinachosemekana kuwa ni kuingilia mambo ya ndani ya Iraq na Lebanon.