RAMALLAH: Abbas apendekeza kuundwe baraza la mawaziri la wasomi
18 Oktoba 2006Matangazo
Rais wa Palestina, Mahmoud Abbas, amependekeza kuundwe baraza la mawaziri la mpito litakalojumuisha wasomi, baada ya juhudi za kuunda serikali ya umoja wa taifa kugonga mwamba.
Lakini chama tawala cha Hamas kinasisitiza kwamba serikali ya muungano itakayojumuisha makundi mbalimbali ndilo chaguo zuri.