Pacquiao aendelea kuuguza jeraha la bega
20 Julai 2015Pacman amesema aendelea kuliuguza jeraha hilo mwenyewe. Arum alimshambulia bondia wake huyo mwishoni mwa wiki akisema hana habari zozote kuhusu ni lini “Pacman” huenda akapanda tena ulingoni baada ya kuumia bega lake la kulia wakati wa pigano na Floyd Mayweather mwezi Mei.
Pacquaio amesema anamheshimu Arum maana yeye ni kama baba yake. Na anaamini kuwa promota huyo anaelezea tu wasiwasi wake kumhusu na hivyo anashukuru hilo na halichukulii kwa ubaya. Lakini hana sababu yoyote ya kuwa na hofu kuhusiana na jeraha lake maana anaendelea kupata nafuu haraka sana kuliko ilivyotarajiwa.
Na kufikia hapo ndipo nakamilisha michezo kwa sasa kwa mengi zaidi, tembelea ukurasa wetu wa michezo, fungua dw.com/Kiswahili, na pia unaweza kuwasiliana nami kupitia facebook na Twitter mimi ni Bruce Amani. Kwaheri
Mwandishi: Bruce Amani/AFP/APE/DPA/Reuters
Mhariri:Josephat Charo