1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

NEW YORK: Mashambulizi ya Irak yalaaniwa vikali

17 Agosti 2007
https://p.dw.com/p/CBYW

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelaani vikali mashambulizi manne yaliyofanywa kwa wakati mmoja,kaskazini mwa Irak.Mashambulizi hayo ya kujitolea muhanga yameua watu wasiopungua 400. Taarifa iliyotolewa na baraza hilo imesema,azma ya mashambulizi hayo ni kuzitenga zaidi jamii za kidini na kikabila nchini Irak.

Mashambulio hayo yalilenga vijiji wanakoishi waumini wa madhehebu ya kale ya Yazidi na yamesababisha idadi kubwa sana ya vifo.