Waswahili husimiliana visa na mikasa iliyopita kwenye maisha na wakati mwengine wakitumia visa vya wanyama, wadudu, miti au maumbile kuelezea sababu au asili ya kutokea jambo fulani. Kwenye wasaa huu wa Kiswahili Kina Wenyewe, Mohammed Khelef anazungumza na Mhadhiri wa Fasihi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dokta Elizabeth Gwajima.