1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mzozo ndani ya chama cha wananchi CUF Tanzania

12 Desemba 2011

Wachunguzi wa mambo ya siasa huko Tanzania wananukuliwa wakisema kwamba mambo si shwari ndani ya uongozi wa chama cha upinzani cha CUF.

https://p.dw.com/p/13R34
CUF’s Sansibar Präsidentschaftskandidat, Seif Sharif Hamad, beim Gespräch mit Journalisten, nachdem der das Formular für seine Kandidatur bei der Sansibar Wahlkommission (ZEC) abholte (5.Juni 2010) Stichwort: Sansibars Präsidentschaftskandidat, Zanzibar Presidential Candidate, Seif Sharif Hamad
Makamo wa kwanza wa rais wa Zanzibar na Katibu Mkuu wa chama cha CUF Seif Shariff HamadPicha: DW

 Mbunge wa chama hicho kutoka Wawi, Pemba, Hamad Rashid Mohamed, ameulaumu vikali uongozi na mwenendo wa chama hicho, akisema katibu mkuu wa chama, Maalim Seif Shariff Hamad, ambaye pia ni makamo wa kwanza wa rais wa Zanzibar, inafaa aache dhamana ya ukatibu mkuu wa chama. Duru za wachambuzi wa mambo zinasema mwenyewe Rashid Hamad Mohammed anafanya kampeni ya kuwashawishi wanachama wa chama cha CUF wamchague yeye kuwa katibu mkuu.

Kupata zaidi juu ya mfarakano huu katika uongozi wa CUF, Othman Miraji  alizungumza na makamo wa katibu mkuu wa CUF, upande wa Visiwani Zanzibar, ambaye pia ni mwakilishi wa mji mkongwe, Ismail Jussa. Alisimulia hivi kuhusu mkasa huo..

Mwandishi: Othman Miraji

Mhariri: Mohamed Abdulrahman