1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mwandishi apigwa risasi Somalia

30 Mei 2013

Watu waliokuwa na silaha wamempiga risasi na kumjeruhi vibaya mwandishi mmoja waandishi wa habari nchini Somalia, katika eneo tete lililopo kusini mwa mji wa bandari wa Kismayo.

https://p.dw.com/p/18hIf
An Ethiopian soldier radios headquarters upon the arrival in the port city of Kismayu after dislodging Islamic fighters from their last remaining stronghold in Somalia on Monday 1 January 2007. Government forces backed by Ethiopian troops took control Somalia's third largest city when soldiers from the Islamic Courts Union abandoned their positions after a night of heavy shelling and advanced with tanks, aircraft and a large contingent of troops. Witnesses report seeing hundreds of Islamic fighters many of them Arabs and South Asians fleeing the town in the direction of neighboring Kenya. Ethiopian troops officially entered Somalia on 24 December, joining fighters loyal to Somalia's interim government, to repel an Islamist assault on the government stronghold of Baidoa. EPA/IBRAHIM ELMI +++(c) dpa - Report+++
Wapigaji wa kiislamuPicha: picture-alliance/dpa

Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, habari za tukio hilo zimetolewa na maafisa wa serikakali na waandishi wengine wa habari nchini humo. Mwandishi mmoja wa habari, mwakilishi wa kituo cha televisheni kinachoitwa Royal TV, chenye ofisi zake kuu mjini London, huko Uingereza alisema washambuliaji wasiojulikana walimshambulia Abdikadir Abdirasak Sofe, ambae pia anajulikana kwa jina la utani "Jijile".

Mkasa huo ulitokea wakati mwandishi huyo akirejea nyumbani kutoka kazini jana jioni. Shuhuda mmoja Ali Mohamed alisema watu wawili mmoja miongoni mwao akiwa ameshika bunduki aina ya AK-47, alimfyatulia risasi majeruhi.

Imeripotiwa mwandishi, Abdikadir Abdirasak Sofe ambae amejeruhiwa mara kadhaa kwa risasi katika maeneo ya juu ya mwili wake, alikimbizwa hospitali. Hata hivyo Mohamed Saleban ambae ni afisa wa jeshi mjini Kismayo amesema baadae watu ambao wanatuhumiwa kuhusika na jaribio hilo la mauwaji walitiwa mbaroni ingawa haikuweza kufahamika mara moja ni nini hasa ilikuwa nia yao.

FILE - In this Wednesday, Dec. 14, 2011 file photo, two Kenyan army soldiers shield themselves from the downdraft of a Kenyan air force helicopter as it flies away from their base near the seaside town of Bur Garbo, Somalia. Kenya's military said Friday, Sept. 28, 2012 that its troops attacked Kismayo, the last remaining port city held by al-Qaida-linked al-Shabab insurgents in Somalia, during an overnight attack involving a beach landing. (Foto:Ben Curtis, File/AP/dapd).
Walinzi wa amani mjini KismayoPicha: AP

Somalia ni moja kati ya maeneo hatari zaidi kwa waandishi wa habari ambapo kiasi ya waandishi 18 waliuwawa mwaka uliopita. Mohamed Ibrahim, kutoka umoja wa waandishi wa habari nchini humo alisema wanaalani vikali vitendo vya kuwafyatulia risasi waandishi habari.

Shambulio dhidi ya Sofe linafuatia mauwaji mengine ya waandishi habari wanne yaliyotokea mwaka huu. Somalia imevurugwa na mgogoro wa tangu mwala 1991, lakini serikali mpya iliyokuwa ikiungwa mkono na iliingia madarakani mwaka uliopita.

Hata hivyo, shambulio la mwandishi Sofe limefanyika katika eneo la kusini la bandari ya Kismayo, ambalo lipo katika mamlaka ya mtu aliyejitangaza kuwa rais wa kanda hiyo ambae ni mshirika wa majeshi ya Kenya yaliyomo katika operesheni ya ulinzi wa amani ya Umoja wa Afrika katika eneo hilo.

Mwaka uliyopota wanamgambo wa Al-Shebab, ambao wana mfungano la mtandao wa kigaidi wa Al-Qaeda walifurushwa na majeshi ya Kenya na washirika wake wa Somalia katika mji wa Kismayo, ingawa bado kumekuwa na matukio ya mashambulizi ya kupangilia katika mji huo.

Sambamba na hayo bado kuna mapambano ya wapiganaji wa makundi ya kikabilia katika eneo la kusini mwa Jubaland ambalo kila kundi linawania kupata fursa ya udhibiti wa kiutawala ya eneo hilo.

Mwandishi: Sudi Mnette AFP
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman