Mpatanishi mkuu wa Iran katika mazungumzo ya Nuklia ajiuzulu
20 Oktoba 2007Matangazo
Msemaji wa serikali Gholam Hossein Elham amesema Ali Larijani ambaye ni katibu wa baraza kuu la usalama la Iran amejiuzulu lakini hakuna sababu zilizotolewa kutokana na uamuzi huo ingawa msemaji wa serikali amesema bwana Larijani anataka kujishughulisha na masuala mengine ya kisiasa.
Rais Mahmoud Ahmedinejad amekubali kujiuzulu kwa Larijani na naibu waziri wa mambo ya nje anayehusika na masuala ya Ulaya na Marekani Saeed Jalili ndiye atakayechukua mahala pake.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali wa Iran mazungumzo kati ya mjumbe wa Iran na mkuu wa sera za nje za Umoja wa ulaya Javier Solana yaliyopangiwa kufanyika jumanne yataendelea kama ilivyopangwa huko mjini Roma Italia.