1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MOSCOW: Mwandishi habari Anna Politkovskaya akumbukwa nchini Urusi

7 Oktoba 2007
https://p.dw.com/p/C7Hn

Wanaharakati kadhaa wanaotetea haki za binadamu walitiwa ndani kwa muda katika mji wa Nishni- Novgorov nchini Urusi.

Wanaharakati hao kutoka nchi za nje walikuwa wanakusudia kushiriki katika mkutano wa hadhara ili kumkumbuka mwandishi habari wa kirusi , Anna Politkovskaya alieuawa kwa kupigwa risasi mjini Moscow mwaka moja uliopita. Mwandishi huyo alikuwa mkosoaji mkali wa serikali.

Shirika la haki za binadamu-Human Rights First limesema kuwa watu hao walikamatwa kwa madai kwamba walikiuka taratibu za viza.