Mjini Mombasa mshukiwa mmoja wa Ugaidi aliyejisalimisha kwa polisi amefikishwa mahakamani. Na washukiwa 42 wa kundi lililopigwa marufuku la Mombasa Republican Council, MRC, pia walikuwa kizimbani kujibu mashtaka ya kupanga njama za kutenda maovu mjini Mombasa.