1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa Shirika la Kazi duniani ILO mjini Addis Abeba,Ethiopia

26 Aprili 2007

Ukosefu wa ajira kwa watu wengi barani Afrika ni changamoto kubwa kwa serikali pamoja na jamii kwa ujumla. Lakini kinachotakiwa si kuongeza nafasi za ajira tu, bali pia ajira hizo ziwe na hadhi kwa wafanyakazi.

https://p.dw.com/p/CB4S
Hilo ni moja kati ya masuala yanayozungumziwa kwenye mkutano wa shirika la Kazi duniani ILO kwa kanda la Afrika, ambao unamalizika leo mjini Addis Abeba,Ethiopia. Tanzania ni nchi moajwapo ambayo imechaguliwa kutoa uzoefu wake katika kutafuta hizo ajira zenye hadhi. Lakini je ajira zenye hadhi,maana yake nini? Suali hilo aliliuliza mwandishi wetu wa Addis Abeba,Anaclet Rwegayura, na Daktari Ladislav Kombe, katibu mkuu wa wizara ya kazi na ajira ya Tanzania ambaye anahudhuria mkutano wa ILO anajibu suali hilo.