1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano kuhusu Ugonjwa wa Malale wafanyika mjini Kampala

21 Septemba 2009

<p>Ugonjwa wa malale unaowaathiri binadamu na ambao pia huwakumba wanyama ungali changamoto kubwa barani Afrika kwa sababu ugonjwa huo husababisha kifo na vile vile ni mgumu kuutibu.

https://p.dw.com/p/JlnO
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), idadi kubwa ya wakaazi  barani Afrika wanaugua ugonjwa wa malale wengi wao wakiwa kwenye maeneo ambayo yamo karibu na wanyama pori au kwenye jamii za wafugaji. Wataalam wa ugonjwa huo, wanasayansi, wanasiasa na mashirika ya kimataifa walikutana hii leo mjini Kampala nchini Uganda kujadili ni vipi watakavyokabiliana na changamoto za ugonjwa huo na hukakikisha unasahaulika barani Afrika. Mwandishi wetu mjini Kampala, Leylah Ndinda  anaripoti zaidi.

Mpitiaji: Grace Patricia Kabogo

Mhariri:Mohamed Abdul-Rahman