Kiswahili kina utajiri mkubwa wa misemo, methali na simo, ambazo licha ya kufumbata ujumbe mzito ndani yake, pia hutumiwa na Waswahili wenyewe kuakisi maisha na mazingira yao. Kwenye sehemu hii ya Kiswahili Kina Wenyewe, Mohammed Khelef anazungumza na mtaalamu wa misemo ya Kiswahili, Bwana Mohammed Said wa Mjini Unguja, ambaye anaufafanua msemo "Usiuchezee upepo wa Kusi kwa tanga bovu".