1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Minsk. Ahmedinejad yuko ziarani Belarus.

21 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CBzt

Rais Alexander Lukashenko wa Belaruss amemuahidi rais mwenzake wa Iran Mahmoud Ahmedinejad kuwa nchi hizo mbili zitashirikiana katika nyanja zote.

Kiongozi huyo wa Iran yuko katika jimbo hilo la zamani la Urusi kwa ziara ya siku mbili.

Wakati wa ziara yake viongozi hao wawili wanatarajiwa kujadili kuhusu nishati, biashara na masuala ya teknolojia.

Lukashenko amekuwa muungaji mkono mkuu wa mpango wenye utata wa kinyuklia wa Iran, wakati Ahmedinejad amemsifu rais huyo wa Belaruss, ambaye anashutumiwa na Marekani kuwa ni dikteta wa mwisho katika bara la Ulaya.

Belarus imekuwa ikihitaji washirika wapya wa kibiashara kutoka nje kwasababu ya hali mbaya ya uhusiano na mshirika wake mkuu wa kiuchumi Russia.