Mfumo wa elimu nchini Tanzania
22 Aprili 2013Utaratibu huo utakaoanza mwaka huu wa masomo 2013/14, utakuwa ukiwahusisha wale ambao elimu yao imeishia darasa la saba na kuendelea, lakini walikosa sifa ya kuendelea na masomo kwa ngazi ya chuo kikuu.
Kupitia utaratibu huo mpya, mtahiniwa atajiunga na Chuo Kikuu kulingana na fani atakayoiomba na atatakiwa kufanya mitihani mitatu na kufaulu kwa wastani wa daraja la B. Hata hivyo hayo yamezusha mjadala miongoni mwa baadhi ya watu wakihoji kwamba tayari mfumo wa elimu uko katika hali mbaya, hasa kutokana na matokeo ya mwaka huu ya mtihani wa kidato cha nne. Amina Abubakar amezungumza na Mdau wa Elimu anayefanya kazi na shirika la "Haki elimu" nchini Tanzania Nyanda Shuli, ambaye kwanza anaelezea maoni yake juu ya hatua hiyo.Kusikiliza mazungumzo hayo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini
Mwandishi: Amina Abubakar
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman