Mazungumzo ya kitaifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kati ya serikali na upinzani yaliyokuwa yatiwe saini jana usiku, yamekwama, huku Kanisa Katoliki likitangaza kujiondoa kuwa mpatanishi katika mazungumzo hayo. Aidha vijana wafuasi wa upinzani wameweka vizuizi katika barabara anakoishi Felix Tshisekedi, aliyekuwa anapendekezwa na upinzani kuwa waziri mkuu wa utawala wa mpito.