Umoja wa Ulaya wapinga msimamo wa Rais wa Marekani Donald Trump kuhusu makubaliano ya Nyuklia ya Iran. Upinzani nchini Kenya unasisitiza hakutokuwa na uchaguzi tarehe 26 Oktoba kama ilivyotangazwa. Kiongozi wa upinzani bungeni nchini Uganda Winnie Kiiza amemshtumu rais Museveni kwa matamshi yake ya kuwatisha wale wanaopinga kubadilishwa kwa katiba ili kuondoa ukomo wa umri wa rais.