1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Marekani: Polisi ya Kenya kukabiliana na uhalifu Haiti

Bruce Amani
2 Agosti 2023

Marekani imesema itawasilisha azimio kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambalo litaidhinisha Kenya kuongoza kikosi cha kimataifa cha polisi kusaidia kupambana na magenge ya uhalifu nchini Haiti.

https://p.dw.com/p/4Ug4J
Kenia wartet mit Spannung auf das Urteil des Obersten Gerichtshofs zu den Wahlen
Picha: Yasuyoshi Chiba/AFP

Magenge hayo yanalidhibiti eneo kubwa la mji mkuu na yanasambaa kote katika taifa hilo la Caribbean. Balozi wa Marekani Linda Thomas-Greenfield amesema Marekani inaukaribisha uamuzi wa Kenya kuongoza kikosi hicho cha kimataifa. Waziri Mkuu wa Haiti Ariel Henry alituma ombi la dharura Oktoba mwaka jana la kupelekwa haraka jeshi maalum, katika kiwango kinachofaa kuyakomesha magenge. Kenya ni nchi ya kwanza kuitikia wito huo, ikisema iko tayari kupeleka maafisa 1,000 wa polisi kusaidia kutoa mafunzo na kulisaidia jeshi la polisi la Haiti kurejesha utulivu nchini humo na kuyalinda maeneo ya kimkakati.