1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Makubaliano yafikiwa Cote d'Voire na wanajeshi

Sekione Kitojo
9 Januari 2017

Rais wa Cote d'Ivoire amesema makubaliano yamefikiwa Jumamosi (07.01.2017)kumaliza uasi wa jeshi wa siku mbili ambao ulirejesha  hali ya wasi wasi wa usalama katika taifa hilo linaloongoza kwa zao la kakao duniani .

https://p.dw.com/p/2VT5R
Elfenbeinküste | Präsident Alassane Ouattara spricht während der offiziellen Zeremonie der Verkündung der dritten Republik der Elfenbeinküste nach dem Referendum über eine neue Verfassung
Rais wa Cote d'Ivoire Alassane OuwattaraPicha: REUTERS/T. Gouegnon

Rais Alassane Ouattara  alisema  hayo  wakati  wa   mkutano  wa baraza  la  mawaziri  siku  ya  jumamosi  jioni. Hapo  mapema , waziri wake  wa  ulinzi Alain-Richard Donwahi , aliongoza  ujumbe  wa majadiliano  pamoja  na  wanajeshi  hao  wanaolalamika  katika  mji wa  pili  kwa  ukubwa  nchini  humo, Bouake, ambako uasi  ulianzia Ijumaa  asubuhi  na  kushuhusia  wanajeshi  wakifyatua  risasi hewani.

Elfenbeinküste Meuternde Soldaten halten Verteidigungsminister fest
Msemaji wa wanajeshi walioasi Picha: Getty Images/AFP/S. Kambou

Lakini  katika  ishara  za  mapema  kwamba  si  kila  mwanajeshi alikuwa  akishiriki  uasi  huo, waasi  mjini  Bouake walianza  kufyatua tena bunduki  zao  za  Kalashnikov  pamoja  na  silaha  nyingine baada  ya  tangazo  la  Ouattara, na  kusababisha  Donwahi kukamatwa  na  kuwekwa  katika  nyumba  ya  afisa  wa  mji  huo pamoja  na  ujumbe  wake  na  waandishi  habari.

Kundi  hilo hatimaye liliweza  kuondoka  kabla  ya  saa  kumi  jioni, alisema  mmoja  wa  mateka , Aboubakar Al Syddick, mwandishi habari  wa  gazeti la  mjini  Abidjan  la   L'Intelligent. Wizara  ya  ulinzi baadaye  ilitoa  taarifa  ikikana  kwamba  Donwahi  alikamatwa kinyume  bna  matakwa  yake, ikisema  alikuwa  tu  akiendelea kufanya  majadiliano.

Wanajeshi watakidhiwa  matakwa yao

Katika  tangazo  lake , Ouattara  alisema  yuko  tayari  kutilia maanani  madai  ya  wanajeshi  hao wanaodai  fedha  zaidi  na mazingira  mazuri  katika  maeneo  wanayoishi  pamoja  na  kazini, lakini  alikosoa  mbinu  walizotumia  za  uasi.

"Nataka  kusema  kwamba  njia  hii  ya  kudai  si  sahihi. Kwa  kweli , inachafua  taswira  ya  nchi  yetu  baada  ya  juhudi  zetu  zote za maendeleo  ya  kiuchumi  na  kujijengea  nafasi  ya  kidiplomasia," alisema.

Elfenbeinküste Meuternde Soldaten halten Verteidigungsminister fest
Wanajeshi walioasi walimshikilia waziri wa ulinzi kwa mudaPicha: Getty Images/AFP/S. Kambou

Ouattara  aliingia  madarakani  mwaka  2011  baada  ya  mzozo  wa baada  ya  uchaguzi  ambao  ulisababisha  zaidi  ya  watu  3,000 kuuwawa.

Mzozo  huo  ulizushwa  na  kukataa  kwa  rais  wa  zamani  wa  nchi hiyo Laurent Gbagbo  kukubali  kushindwa   na  kujiuzulu. Machafuko hayo  yalifikisha  kilele  cha  mzozo  uliokuwa  ukitokota  wa  zaidi  ya muongo  mmoja  ambao  ulianza  kwa  mapinduzi  ya  kwanza  nchini humo  mwaka  1999.

Mzozo  huo sio  mwisho wa  matatizo

Rais huyo mpya  anakabiliwa  na  changamoto  nyingi  katika  kujaribu kujenga  jeshi la  pamoja. Wadadisi  wa  masuala  ya  kisiasa walitabiri  serikali  itatoa  fedha  ili  kuzima  mzozo  wa  wiki  hii, kama ilivyofanya  wakati  wanajeshi  walipofanya  uasi  kama  huo mwaka 2014.

Elfenbeinküste Meuternde Soldaten halten Verteidigungsminister fest
Wanajeshi wa Cote d'Ivoire walioasiPicha: Getty Images/AFP/S. Kambou

Maelezo  kuhusiana  na  makubaliano  hayo  hayakupatikana  mara moja. Licha  ya  juhudi  hizo  za  serikali  kupata  suluhisho  la haraka, tukio  hilo  linaelekeza  katika  matatizo  yanayoendelea kuwapo  katika  Cote d'Ivoire  inayojitoa  kutoka  katika  matatizo, amesema Cynthia Ohayon, mchambuzi  wa  masuala  ya  kisiasa  wa Afrika  magharibi  kwa  ajili  ya  kundi  la  kimataifa  linaloangalia mizozo.

"Hii  ni tukio  jingine  linalokumbusha  kwamba  masuala  ambayo bado  yapo ambayo  yalisababisha  mzozo bado  hayajatatuliwa," amesema. "Baadhi  ya  watu  wanasahau  na  wanafikiri  kwamba kila  kitu kinakwenda  vizuri  nchini  Cote d'Ivoire. Nafikiri  hali  hii inapaswa  kupunguzwa."

Mwandishi : Sekione  Kitojo / ape

Mahariri: Isaac Gamba