1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Majadiliano ya bajeti yakwama

10 Novemba 2012

Juhudi za mwanzo za kupatikana makubaliano juu ya bajeti ya mwaka 2013 ya umoja wa Ulaya zimeshindwa.

https://p.dw.com/p/16gQO
ARCHIV - Arbeiter demontieren in der Nacht von Donnerstag (16.08.2012) am Flughafen in Frankfurt am Main eine Euro-Skulptur am Terminal. Die Verhandlungen über den EU-Haushalt des kommenden Jahres sind am Freitagabend in Brüssel gescheitert. Dies teilte ein Sprecher der EU-Kommission mit. Die Vertreter der 27 EU-Regierungen und des Europaparlamentes trennten sich ergebnislos. Foto: Fredrik von Erichsen dpa/lhe +++(c) dpa - Bildfunk+++
Bunge la Ulaya lajadili bajeti ya mwaka 2013Picha: picture-alliance/dpa

Serikali za mataifa ya umoja huo pamoja na bunge zimeshindwa kupata msimamo wa pamoja kuhusu suala la utendaji baada ya karibu saa nane za mazungumzo jana Ijumaa(09.11.2012).

Pande hizo mbili zitajaribu tena kupata makubaliano siku ya Jumanne, kabla ya muda wa mwisho ambao ni usiku wa manane , kuweza kukubaliana juu ya bajeti ama kuirejesha halmashauri ya Ulaya , katika kazi ya kuipanga upya bajeti hiyo.

Wanasiasa wa umoja wa Ulaya hawatilii manani sana uchelewesho huo, na wana matumaini kuwa muda wa mwisho unaweza kufikiwa.

European Union member states' flags flutter in the wind, in front of the building of the European Parliament in Strasbourg, in this file photo taken April 21, 2004. The European Union won the Nobel Peace Prize for its long-term role in uniting the continent, the Norwegian Nobel Committee said on Friday, an award seen as morale boost for the bloc as it struggles to resolve its debt crisis. The committee praised the 27-nation EU for rebuilding after World War Two and for its role in spreading stability to former communist countries after the 1989 fall of the Berlin Wall. REUTERS/Vincent Kessler/Files (FRANCE - Tags: POLITICS)
Bunge la Ulaya katika mji wa Straßburg nchini UfaransaPicha: Reuters

Jumanne ndio mwisho

"Ni pale tu ambapo hatutaweza kufanikiwa siku ya Jumanne, tuwe watulivu na hatupaswi kujiuliza kuhusu nia njema ya wadau wote," amesema Adreas Mavroyiannis, naibu waziri anayehusika na masuala ya ulaya kutoka Cyprus, nchi ambayo kwa sasa inashikilia urais wa kupokezana wa umoja wa Ulaya.

"Inatokea katika wakati wa muafaka kuwa kuna kuwa na hali ya mkwamo , wasi wasi," amesema kamishna wa bajeti ya umoja wa ulaya Janusz Lewandowski. "lakini nafikiri hali ya uwajibikaji ipo."

Janusz Lewandowski, EU-Kommisär für Finanzprogrammierung und Budget seit 2010, Privatisierungsminister Polens 1991 und 1992-93 Autor: Aureliusz M. Pędziwol
Kamishna wa Ulaya anayehusika na bajeti Janusz LewandowskiPicha: Aureliusz Marek Pędziwol

Mavroyiannis, hata hivyo , amesema kuwa hali ya kuweza kushindwa siku ya Jumanne "haiwezi kuondolewa kabisa".

Mkwamo ukizidi ni hatari

Kabla ya mazungumzo hayo ya jana Ijumaa(09.11.2012) , maafisa wa serikali za umoja wa Ulaya wameonya kuhusu hatari ya kuendelezwa kwa mazungumzo hayo hadi kuingia katika mwaka 2013, kabla ya kuanza kwa majadiliano juu ya bajeti ya mwaka 2014 hadi 20 katika muda wa wiki mbili.

"nafikiri itatoa ishara mbaya sana iwapo tutaendelea kuvutana kuhusiana na masuala haya," amesema Brian Hayes waziri wa fedha wa Ireland.

Serikali za mataifa ya umoja wa Ulaya pamoja na bunge la Ulaya zinatofautiana kwa mbali sana kuhusiana na kiasi gani kitumiwe mwaka ujao.

Mataifa wanachama yanataka bajezi inayofikia kiasi cha euro bilioni 132.7 ama ongezeko la asilimia 2.8.

Serikali za kihafidhina zinazoangalia sana masuala ya bajeti kama Ujerumani, Uholanzi na Denmark yanasisitiza kuwa kiwango hicho kikubalike, suala ambalo pia linaungwa mkono na Ufaransa na Uhispania, na kuweka mataifa matatu yenye uchumi mkubwa katika umoja wa Ulaya katika upande mmoja.

"Muktadha ni juu ya kubana matumizi. Serikali ya Uhispania inachukua hatua madhubuti za kubana matumizi. Hii ndio sababu ni muhimu kwa umoja wa Ulaya kuchukua juhudi pia, kuanzisha hatua za kupunguza matumizi," balozi wa Uhispania katika umoja wa Ulaya , Alfonso Dastis amesema.

Lakini wabunge wa umoja wa ulaya wanapigia upatu bajeti itakayofikia kiasi cha euro bilioni 137.9, ama ongezeko la asilimia 6.8, wakidai kuwa fedha hizo zinahitajika ili kuweza kugharamia mipango na miradi ambayo imekubalika hapo kabla.

Mwandishi : Sekione Kitojo / dpae

Mhariri: Stumai George