Eritrea inashika nafasi ya sita au ya saba kwa kuwa na wakimbizi wengi duniani. Wakati inafahamika kwamba watu wanakimbia Syria na Iraq kutokana na umwagaji damu, hali ni tofauti Eritrea. Kipindi cha Mbiu ya Mnyonge kinamulikia sababu za maelfu ya vijana kuikimbia nchi hiyo ya pembe ya Afrika.