1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Madereva wawili wa Shirika la Msalaba Mwekundu wauwawa Sudan

Sudi Mnette
3 Mei 2024

Watu wenye silaha wamewaua madereva wawili na kuwajeruhi wafanyakazi wengine watatu wa Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu huko Sudan.

https://p.dw.com/p/4fSAZ
Jordan Amman | Wahudumu wa ICRC wanatayarisha vifaa vya kibinadamu kwa ajili ya Sudan
Wahudumu wa Msalaba mwekundu wanatayarisha vifaa vya kibinadamu kwa ajili ya Sudan Aprili 30, 2023,Picha: ICRC/AFP

Taarifa ya shirika hilo inaeleza kuwa timu ya wafanyakazi hao ilikuwa njiani ikirejea kutoka Layba kutathmini hali ya kibinadamu ya jamii zilizoathiriwa na vurugu za kutumia silaha katika eneo hilo wakati tukio hilo lilipotokea.

Mzozo kati ya jeshi la Sudan linaloongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan na wanamgambo wanaongozwa na aliyekuwa makamu wake Mohamed Hamdan Daglo umesambaratisha nchi hiyo katika mzozo uliodumu kwa zaidi ya mwaka.

Vita hivyo vimeua maelfu ya watu na kuwalazimu mamilioni ya wengine kuyakimbia makazi yao katika kile ambacho Umoja wa Mataifa umekiita "Mzozo mkubwa zaidi wa watu kuhama makwao duniani."