LONDON: Mwanamfalme wa Uingereza, Philip afanya ziara nchini Irak
23 Oktoba 2006Matangazo
Mwanamfalme wa Uingereza Philip, mumewe Markia Elizabeth wa II, alifanya ziara isiotarajiwa nchini Irak na kuwatembelea wanajeshi wa Uingereza katika mji wa Basra kusini mwa nchi. Makao ya Markia ya Uingereza Buckingham Palace, yamesema mwanamfalme Philip, mwenye umri wa miaka 85 sasa, amewatembelea wanajeshi wa Uingereza wanaomaliza muda wao wa miezi 6 kwenye meli ya Queen’s Royal ambayo ilikuwa ikishika doria kwenye eneo la mpaka kati ya Irak na Iran.
Mwanamfalme Philip ambae ndie kamanda wa heshima wa kikosi hicho cha wanamaji, aliwaambia wanajeshi wa Uingereza kwamba wamefanya kazi kubwa na yenye kupendeza. Alisema raia wa Uingereza wanatambua juhudi wanazozifanya kusaidia kuboresha hali ya mambo nchini Irak.