1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

London. Anayetuhumiwa kumuua Litvinenko atakiwa.

29 Mei 2007
https://p.dw.com/p/CBxD

Uingereza imeiomba rasmi Russia kumpeleka nchini humo mtu anayetuhumiwa kuumuua wakala wa zamani wa Ujasusi wa Russia Alexander Litvinenko.

Maafisa wamethibitisha kuwa balozi wa Uingereza ametoa ombi hilo la kupelekwa kwa Andrei Lugovoi kwa wizara ya mambo ya kigeni ya Russia.

Waendesha mashtaka wa Uingereza wamesema wiki iliyopita kuwa wanataka kumfikisha Lugovoi mbele ya mahakama ya Uingereza na kumshtaki kwa kumpa sumu Litvinenko mjini London Novemba mwaka jana.

Lugovoi amekuwa akikanusha kuhusika katika mauaji ya Litvinenko.

Sheria za Russia zinazuwia kupelekwa raia wake nje ya nchi hiyo.