1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Libya yawakamata wahamiaji 948

25 Juni 2018

Maafisa nchini Libya wanaarifu kuwa askari wa kikosi cha ulinzi wa pwani wamewakamata wahamiaji 948 na kugundua maiti 10 kutoka mataifa ya Kiafrika waliokuwa kwenye boti katika operesheni kadhaa.

https://p.dw.com/p/30DwP
Libyen Tripolis illegale Migranten
Picha: picture-alliance/Xinhua/H. Turkia

Operesheni hizo zilizoanza tangu wiki iliopita, zinafikisha idadi jumla ya wahamiaji hasa wa Kiafrika wanaojaribu kuvuka bahari kwenda Italia lakini wakarejeshwa Libya kuwa karibu 2,000.

Pwani ya magharibi ya Libya ndio njia kuu ya kuondokea kwa maelfu ya wahamiaji wanaokimbia vita na umaskini na kujaribu kuingia barani Ulaya.

Msemaji wakikosi cha jeshi la majini la Libya, Ayoub Qassem, aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa walinzi wa pwani waliwakamata wahamiaji haramu katika makundi tofauti.

Kundi la kwanza lilikuwa na watu 97 na la pili lilikuwa na wahamiaji 361, wakiwa kwenye boti za mipira.