KINSHASA : Ajali ya ndege yauwa 38
5 Oktoba 2007Matangazo
Takriban watu 38 wamekufa wakati ndege ya mizigo iliotengenezwa Urusi ilipoanguka na kuripuka katika mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo Kinshasa.
Watu wengine 30 wamejerubiwa wakati ndege hiyo aina ya Antonov 26 inayoendeshwa na shirika la ndege la Congo Afrika One ilipoangukia nyumba muda mfupi baada ya kuruka kutoka uwanja wa karibu wa kimataifa wa Ndjili.
Maiti zinaendelea kutafutwa kwenye vifusi na idadi ya vifo yumkini ikaongezeka.