Barani Afrika, desturi ya kuwapa majina watoto wanaozaliwa ina mizizi mirefu na mawanda mapana. Inasemekana kuwa takribani kila jina la mtoto wa Kiafrika lina maana na ujumbe maalum unalouwasilisha. Kazi ya kumpa jina mtoto ni shughuli inayofanywa huku wazazi wakiwa na makusudi maalum.