Kibaki akataa kutia saini mswada wa kukandamiza vyombo vya habari
23 Agosti 2007Matangazo
Rais Mwai Kibaki wa Kenya amekataa kutia saini mswada wa sheria juu ya vyombo vya habari.Rais Kibaki amesema mswada huo unahatarisha demokrasi .
Kama rais huyo angetia saini mswada huo na kuwa sheria, sheria hiyo ingezipa mahakama uwezo wa kuwalazimisha waandishi habari kufichua vyanzo vya habari zao.
Rais Kibaki amesema katika tamko kwamba mswada huo ni tishio kwa mafanikio ya demokrasia nchini Kenya.