Kenya: Mwanasiasa mkongwe Martin Shikuku afariki dunia
23 Agosti 2012Matangazo
Shikuku amefariki akiwa na umri wa miaka 79 akipokea matibabu katika Hospitali ya Hurlingham Nairobi.Shikuku alikuwa mbunge wa eneo la Butere Magharibi mwa Kenya hadi mwaka 1997,lakini harakati zake katika mapambano ya kupigania Uhuru ni jambo ambalo halitosahaulika katika fikra za Wakenya.
Saumu Mwasimba amezungumza na Aliyekuwa makamu wa rais wa Kenya bwana Moody Awori ambaye ametoka mbali kisiasa pamoja na mwanasiasa huyo mkongwe na kwanza anaeleza mambo yatakayokumbwa kwa Martin Shikuku.
(Kusikiliza mazungumzo hayo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini)
Mwandishi: Saumu Mwasimba
Mhariri: Othman Miraji