Kemikali Ali ahukumiwa kifo
24 Juni 2007Matangazo
Wanachama wengine wawili wa zamani wa ngazi ya juu katika utawala wa Saddam Hussein pia wamehukumiwa adhabu ya kifo kwa dhima waliyotimiza katika shambulio la mauaji ya kimbari dhidi ya Wakurdi walio wachache nchini Iraq.Watu wengine wawili wamehukumiwa kifungo cha maisha gerezani na mtu wa watano ameachiliwa huru kutokana na kukosekana kwa ushahidi.
Ali Hassan al Majid binamu wa Saddam Hussein amekuwa akihesabiwa kuwa ni mpangaji wa kampeni hiyo ya mauaji ya kimbari.Ametuhumiwa kwa kuamuru mashambulizi hayo kwa kutumia silaha za kemikali dhidi ya wananchi wa Kikurdi walioko kaskazini mwa Iraq na kupelekea vifo vya takriban Wakurdi 180,000.