1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Kansela wa Ujerumani Merkel apambana na maswali ya waandishi

20 Julai 2013

Wiki tisa kabla ya uchaguzi mkuu, kansela Angela Merkel amesalimika maswali magumu ya waandishi habari Ijumaa(19.07.2013)kuhusiana na uchunguzi wa udukuzi uliofanywa na Marekani na jinsi serikali yake ilivyohusika.

https://p.dw.com/p/19B2l
German Chancellor Angela Merkel gestures as she address media during a news conference at Bundespressekonferenz in Berlin July 19, 2013. REUTERS/Tobias Schwarz (GERMANY - Tags: POLITICS)
Kansela Angela MerkelPicha: Reuters

Amesisitiza hata hivyo kuwa bado anasubiri majibu kutoka Marekani kuhusiana na suala hilo.

Merkel anaendelea kuwa mgombea mwenye nafasi ya juu katika uchaguzi utakaofanyika hapo Septemba 22, na uchunguzi mpya wa maoni ya wapiga kura unaonesha kuwa kadhia hiyo ya upelelezi wa mawasiliano ya simu na internet sio suala kuu hadi sasa katika uchaguzi.

German Chancellor Angela Merkel arrives for a news conference at Bundespressekonferenz in Berlin July 19, 2013. REUTERS/Thomas Peter (GERMANY - Tags: POLITICS)
Merkel katika mkutano na waandishi habari mjini BerlinPicha: Reuters

Matumaini ya wapinzani

Lakini upinzani una matumaini kuwa hali hiyo huenda ikabadilika kwa kuwa vyombo vya habari vinaelekea kulichukulia suala hilo kwa nguvu.

Akishinikizwa na maswali kuhusu mpango wa usalama wa taifa nchini Marekani wa PRISM kwa muda wote wa dakika 100 za mkutano wake wa kila mwaka na waandishi habari wakati wa majira ya joto, Merkel ameendelea kusema kuwa amefahamu kuhusu suala hilo kupitia vyombo vya habari, na hana taarifa za kina na ameomba kuwepo uvumilivu.

Merkel amesisitiza kuwa nchi yake , "sio taifa la kufanyiwa uchunguzi" na kwamba "sheria za Ujerumani zinatakiwa kutumika katika ardhi ya Ujerumani" lakini pia amekiri kuwa hali hiyo ina mipaka yake katika enzi hizi za mfumo wa mawasiliano ya dunia.

Former intelligence agency contractor Edward Snowden speaks to human rights representatives in Moscow's Sheremetyevo airport July 12, 2013. Snowden is seeking temporary asylum in Russia and plans to go to Latin America eventually, an organisation endorsed by anti-secrecy group Wikileaks said on Twitter on Friday. REUTERS/Human Rights Watch/Handout (RUSSIA - Tags: POLITICS PROFILE CRIME LAW TPX IMAGES OF THE DAY) NO COMMERCIAL OR BOOK SALES. NO SALES. NO ARCHIVES. FOR EDITORIAL USE ONLY. NOT FOR SALE FOR MARKETING OR ADVERTISING CAMPAIGNS - eingestellt von : ml
Edward SnowdenPicha: Reuters

Mbinyo umeongezeka kwa wiki kadha dhidi ya Merkel kuhusiana na madai ya upelelezi yaliyotolewa na mfanyakazi wa shirika la ujasusi la Marekani anayetafutwa Edward Snowden, ambaye pia amesema shirika la ujasusi la Ujerumani BND lilishiriki pamoja na shirika hilo la usalama wa taifa nchini Marekani kufanya uchunguzi huo.

Merkel kavunja kiapo

Upinzani wenye nadharia za wastani za mrengo wa shoto umedai kuwa Merkel amevunja kiapo chake cha kuongoza nchi kwamba atalinda haki za raia za mawasiliano ya binafsi , suala ambalo ni nyeti kutokana na historia ya shughuli za askari kanzu chini ya utawala wa Wanazi pamoja na ule wa Ujerumani ya mashariki ya kikomunisti.

Uchunguzi uliofanywa na kituo cha televisheni ya taifa cha ARD umegundua kuwa zaidi ya theluthi mbili ya wapiga kura wa Ujerumani hawaridhishwi na juhudi za serikali kuufahamisha umma juu ya suala hilo.

Hata hivyo , uchunguzi huo huo pia umesema kuwa, takriban kwa sasa, hali hiyo haijabadilisha nafasi ya uongozi aliyonayo kansela Merkel wakati nchi hiyo inaelekea katika likizo za majira ya joto, na kwamba theluthi mbili ya Wajerumani wanasema suala hilo halitaathiri kwa kiasi kikubwa matokeo ya uchaguzi.

Mafanikio ya Merkel

Kansela amesisitiza mafanikio yake katika kuushughulikia uchumi pamoja na jinsi alivyoshughulikia mafuriko ya hivi karibuni , na amesema kuwa serikali yake inayoundwa na vyama vya nadharia za wastani za mrengo wa kulia , kuwa ni ya mafanikio makubwa tangu Ujerumani mbili kuungana mwaka 1990.

BERLIN, GERMANY - OCTOBER 01: German Social Democrats (SPD) Chairman Sigmar Gabriel speaks to the media with German Finance Minister Peer Steinbrueck (not pictured) following a meeting of the SPD Governing Board at SPD headquarters that unaminously confirmed Steinbrueck as the SPD's 2013 candidate for chancellor on October 1, 2012 in Berlin, Germany. Steinbrueck will run against current German Chancellor Angela Merkel in 2013 federal elections. (Photo by Sean Gallup/Getty Images)
Mwenyekiti wa chama cha upinzani cha SPD Sigmar GabrielPicha: Getty Images

Kuhusiana na suala la uchunguzi wa shirika la usalama wa taifa la Marekani NSA, Merkel amezungumzia kitisho cha ugaidi wa kimataifa pamoja na maafa ya kutisha ya Septemba 11 na kusema ni kitu cha kawaida kwa mashirika ya ujasusi kushirikiana, akitaja msaada wa ujasusi wa Marekani hapo zamani kusaidia kujua wahanga raia wa Ujerumani waliotekwa nyara waliko nje ya nchi. Pia amesisitiza kuwa ni muhimu kuwa na mipaka kuhusiana na uchunguzi wa siri wa mataifa, na kwamba katika baadhi ya nyakati , "matokeo hayahalalishi njia ya kupatikana kwake".

Mwandishi : Sekione Kitojo / afpe

Mhariri : Amina Abubakar