Kamata kamata huko Kenya imeanza kushuhudiwa baada ya kiongozi wa upinzani nchini humo Raila Odinga kujiapisha kama rais wa wananchi hapo jana. Tom Kajwang aliyesimamia hatua hiyo ya kujiapisha Raila Odinga ametiwa nguvuni huku Serikali ikisema kuwa watu wengi watakamatwa. Sikiliza ripoti ya mwandishi wa DW Shisia Wasilwa.