KABUL.Wapiganaji 50 wauwawa
26 Oktoba 2006Matangazo
Wanajeshi wa muungano wa NATO wamewauwa takriban wapiganaji 50 wa Taliban katika mapigano makali yaliyozuka kusini mwa Afghanistan.
Kikosi cha ISAF pia kimeanzisha uchunguzi kuhusu madai kwamba raia wameuwawa katika shambulio la ndege wakati wa mapambano.
Wanakijiji wa Panjwayi wamedai kuwa takriban raia 60 wameuwawa katika mlipuko wa bomu. Kikosi cha ISAF kimesema kuwa kinasikitishwa na vifo hivyo vya raia.