KABUL.Polisi auwawa katika shambulio la kujitoa muhanga
26 Februari 2007Matangazo
Mshambuliaji wa kujitoa muhanga amesababisha kifo cha polisi mmoja nchini Afghanistan wakati polisi huyo alipojaribu kumzuia mtu huyo kuingia ndani ya kituo cha polisi.
Mshambuliaji huyo wa kujitoa muhanga alijilipua kwa mabomu aliyokuwa amejizingirisha kwenye mwili wake, watu saba pia wamejeruhiwa katika shambulio hilo katika mji wa Khost mashariki mwa Afghanistan.
Kwa mujibu wa taarifa za jeshi la Marekani takriban raia 200 na wanajeshi kadhaa wa Afghanistan na wale wa kimataifa wameuwawa katika mashambulio ya aina hii.