KABUL: Wapiganaji wa Taliban wauawa kusini mwa Afghanistan
15 Mei 2007Matangazo
Hadi wapiganaji 60 wa Kitaliban wameuawa katika mashambulio ya angani yaliyofanywa na vikosi vya NATO kusini mwa Afghanistan.Polisi katika wilaya ya Kandahar wakitoa taarifa hiyo wamesema, mashambulio hayo yalifanywa wakati wa usiku katika eneo la Zherai,baada ya vikosi vya Afghanistan na NATO kuarifiwa kuwa waasi wa Taliban walikusanyika katika maeneo mawili ya wilaya hiyo.Msemaji wa NATO lakini amesema kwa wakati huu operesheni hiyo haiwezi kuthibitishwa.