KABUL: Shambulio la bomu Afghanistan limeua watu 2
3 Machi 2007Matangazo
Hadi watu 2 wameuawa na 15 wengine wamejeruhiwa katika mripuko wa bomu uliotokea Herat,magharibi mwa Afghanistan.Maafisa wa eneo hilo wamesema, bomu lilitegwa kwenye baiskeli ilioachwa kando ya barabara na liliripuliwa kutoka mbali dakika chache tu baada ya magari mawili ya NATO kupita sehemu hiyo.