1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Jimbo la Wakurd lashutumu mashambulizi ya Uturuki.

18 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/CdAQ

Sulaimania , Iraq.

Serikali ya jimbo lenye madaraka yake ya ndani la Wakurd nchini Iraq leo imeshutumu mashambulizi ndani ya mpaka wa nchi hiyo yaliyofanywa na majeshi ya Uturuki .

Fouad Hussein , mkuu wa ofisi ya rais wa jimbo hilo la Wakurd Mahmoud barzani , amesema kuwa Uturuki inataka kuhamishia matatizo yake katika jimbo hilo la Iraq. Ameongeza kuwa hafahamu ukumbwa wa jeshi la Uturuki ambalo limevuka mpaka na kuingia nchini Iraq.