Imebainika kuwa mitandao ya kijamii ya vyombo vikubwa vya habari vya Ujerumani hujaa kauli za chuki dhidi ya wageni na wahamiaji pindi inapotokea pametumwa taarifa humo kuhusu mashambulizi ya kigaidi ndani ya mataifa ya Ulaya. Kundi la vijana linalotumia hashtag ya #IchBinHier limeamua sasa kupambana na chuki hizo kwa kampeni kali humo humo mitandaoni.