Ghasia zaendelea mjini London
7 Agosti 2011Matangazo
Zaidi ya watu 200 walikusanyika karibu na kituo cha polisi cha Tottenham kabla ya maandamano hayo kugeuka kuwa vurugu. Polisi mjini London imesema, wafanyavurugu waliwarushia chupa maafisa wa polisi waliokuwa kwenye doria na waliyatia moto magari ya polisi na basi moja.
Siku ya alhamisi, tukio la kufyatuliana risasi na polisi, lilisababisha kifo cha mwanaume mwenye umri wa 29. Polisi wanasema, uchunguzi unafanywa kuhusu kifo hicho.
Mwandishi: Sudi Mnette
Prema Martin