Gbagbo angángánia madaraka Cote d´Ivoire
7 Aprili 2011Matangazo
Vikosi hivyo vimekabiliwa na mapigano makali kutoka wafuasi wa mwisho wa Gbagbo, anaepinga kabisa kuondoka madarakani, licha ya jeshi lake kusalim amri Jumanne iliyopita.
Kwa mujibu wa msemaji wa Umoja wa Mataifa, majadiliano yanafanywa pamoja na Gbagbo lakini kiongozi huyo binafasi ameiambia stesheni moja ya redio ya Ufaransa kuwa hana azma ya kuondoka madarakani.
Umoja wa Ulaya unamlaumu Gbagbo kusababisha umwagaji damu huu mpya na umeweka vikwazo vipya dhidi ya Gbagbo, kwa kupiga marufuku kununua hisa za serikali yake. Umoja wa Ulaya umeshaweka vikwazo kadhaa dhidi ya Gbagbo na washirika wake, baada ya kiongozi huyo kukataa kutambua matokeo ya uchaguzi wa Novemba mwaka jana na kuondoka madarakani kufuatia.