1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Gazeti la Marekani lamsifu Putin

20 Desemba 2007
https://p.dw.com/p/Ce94

WASHINGTON.Gazeti la Time la Marekani, limemtaja Rais wa Urusi Vladmir Putin kama , ni mtu mashuhuri wa mwaka.

Gazeti hilo limesema kuwa uamuzi huo umetokana na hatua za Putin zilizoibadilisha Urusi kuwa nchi muhimu katika karne ya 21.

Limesema kuwa Putin amekuwa imara na kuiimarisha nchi hiyo hali ambayo huko nyuma haikuwahi kuwa nayo.