Fahamu WhatsApp inavyoshamiri kwenye mashirika makubwa
Yusra Abdallah Buwayhid24 Februari 2016
Je, umeshawahi kukasirishwa na kampuni kwa huduma yao mbaya kwa wateja? Labda kwa kuwa ukipiga simu hawapokei. Ama ukiwatumia barua pepe kuwaelezea tatizo lako kama mteja, huwa wanachukuwa muda mrefu hadi kukujibu. Tatizo hilo sasa linaweza kurahisishwa kupitia majukwaa ya ujumbe wa papo hapo. Ungana na Yusra Buwayhid akizungumza na kampuni ya Ongair ya Kenya inayojihususha na huduma hiyo.