Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imetangaza kuanzishwa uchunguzi baada ya kusambaa kanda ya vidio kwenye mitandao ya kijamii, inayoonyesha wanajeshi wakiwauwa wapiganaji wa kikabila wasiokuwa na silaha. Na, kanisa katoliki la mji mkuu Kinshasa, limeshambuliwa kwa tuhuma kwamba maaskofu ambao ni wapatanishi katika mgogoro wa kisiasa nchini humo wameshindwa kumaliza mazungumzo hayo.