Dominique Strauss-Kahn aachiliwa huru kwa mashtaka ya ngono
24 Agosti 2011Matangazo
Jaji Michael Obus alilikubali ombi la mwendeshaji mashtaka la kuachana na kesi hiyo ambayo wameiona haiwezekani kushinda kutokana na mshtaki- mtumishi wa hoteli, Nafissatou Diallo, aliyemtuhumu Strauss-Kahn kufanya nae ngono kwa nguvu- kuwa alisema uwongo mara kadhaa, hivyo haaminiki. Strauss-Kahn, akitoka mahakamani na mkewe, Anne Sinclair, ambaye katika wakati wote tangu kashfa hiyo kujulikana, amemtea mumewe na kusema hana hatia, alisema amepumua na kumshukuru mkewe, watoto wake na kila mtu aliyemuunga mkono. Punde hivi Othman Miraji alizungumza na mwandishi wa habari wa mjini Paris, Mohammed Saleh, juu ya vipi wafaransa walivopokea habari za kuachiliwa huru Dominique Strauss-Kahn...
Mwandishi: Othman Miraji
Mhariri: Mohamed Abdulrahman