1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

CONAKRY.Maelfu ya watu washiriki kwenye maandamano

12 Februari 2007
https://p.dw.com/p/CCT2

Takriban watu watatu wameuwawa kufuatia maandamano makubwa katika miji ya Conakry na mji wa mashariki wa Kankan nchini Guinea.

Maelfu ya watu wameandamana huku waporaji wakitumia vurugu hizo kuvunja maduka na kupora mali.

Mgomo ulioitishwa na viongozi wa vyama mbalimbali umeathiri sehemu nyingi za taifa hilo la Afrika Magharibi katika juhudi za kutaka kumng’oa mamlakani waziri mkuu Eugene Camara ambae ni chaguo la rais Lansana Conte.